Hebrews 10:1-6

Dhabihu Ya Al-Masihi Ni Mara Moja Tu

1 aTorati ni kivuli tu cha mambo mema yajayo, wala si uhalisi wa mambo yenyewe. Kwa sababu hii, haiwezekani kamwe kwa njia ya dhabihu zitolewazo mwaka hadi mwaka kuwakamilisha wale wanaokaribia ili kuabudu. 2 bKama dhabihu hizo zingeweza kuwakamilisha, hazingeendelea kutolewa tena. Kwa kuwa hao waabuduo wangekuwa wametakaswa mara moja tu, wala wasingejiona tena kuwa na dhambi. 3 cLakini zile dhabihu zilikuwa ukumbusho wa dhambi kila mwaka, 4 dkwa sababu haiwezekani damu ya mafahali na mbuzi kuondoa dhambi.

5 eKwa hiyo, Al-Masihi alipokuja duniani, alisema: “Dhabihu na sadaka hukuzitaka,
bali mwili uliniandalia;

6 sadaka za kuteketezwa na za dhambi
hukupendezwa nazo.
Copyright information for SwhKC